Posts

Showing posts from 2017

KWA HILI YANGA WAPASWA KUIGA KWA SIMBA

Image
Kilichofanywa na Simba SC ni kitu kikubwa sana katika mpira wetu Tanzania na ni jambo la kupongezwa na kuigwa. Ulimwengu wa soka hivi sasa unasimama katika misuli bora ya kiuchumi. Watu wenye nguvu za kiuchumi na weledi sahihi wa kuuendesha mpira kibiashara ndio watu sahihi kulishika soka letu. Kikubwa Simba ya Mohamedi Dewji ni kusimama vyema kama kielelezo cha soka la kisasa nchini ili vilabu vingine viige na hatamu bora kisoka tuikamate nchini. Big up Simba SC ! leo mmed hihirisha nini maana ya kauli mbiu yenu NGUVU MOJA . Ni nguvu ambayo imelenga katika umoja, ushirikiano, weledi na matamanio chanya kuleta mapinduzi sahihi ya soka nchini. Maamuzi mliyofikia leo endapo LENGO litatimia basi kumbukumbu yenu itajichora kwa wino wa chuma kusomwa na vizazi vingi vijavyo si kwa Simba tu bali kwa watanzania wote katika tasnia ya soka nchini. Neno langu kwenu; samuel samuel

SIMBA KUIBANIA SINGIDA UNITED KWA LUZIO?

Image
HARAKATI za klabu ya Singida United ya Mholanzi Hans Pluijm kumnasa straika wa Simba, Juma Liuzio, ni kama zimegonga mwamba kwa sababu Wekundu hao wa Msimbazi hawataki kumuachia. Singida inamuhitaji Liuzio kwa ajili ya kuongezea nguvu kikosi chake kwenye mzunguko wa pili baada ya kurizishwa na kiwango chake. Rafiki wa karibu wa Liuzio aliiyambia Mkalimangi blog, ni kweli Singida wanamuhitaji mchezaji huyo lakini Simba imeonyesha dalili zote kuwa haitaki kumuachia. "Kweli Singida inamtaka, Liuzio lakini Simba wamegoma, hawataki kumtoa sasa sijui kwa nini wakati wenyewe hawampi nafasi kubwa ya kucheza. Bora wangemtoa akajaribu maisha mengine huko,"alisema. Liuzio mchezaji wa zamani wa Mtibwa Sugar, klabu iliyomlea na kumuuza Zesco ya Zambia, alirudi nchini mwaka jana akasajiliwa kwa mkopo na Simba anayoichezea mpaka sasa

MTAZAMO WA MDAU KUHUSU NGOMA DONALD

Image
Huu ulikuwa usajili makini msimu wa 2015-16 lakini haukuwa usajili sahihi kwa msimu huu. Commitment ni kitu cha msingi sana kazi huonesha heshima na uwajibikaji. Kuna wakati wafanyakazi hutakiwa kulinda ajira zao na masilahi mapana ya taasisi wanayoitumikia. Fedha iliyotumika katika usajili ilipaswa kutafuta wachezaji wenye nidhamu, kujituma , wavumilivu na wenye kuheshimu masilahi ya timu. Ni ukweli usiopingika Ngoma ni mmoja kati ya wachezaji wenye kipaji kikubwa kumvutia  mwalimu yoyote yule lakini anakosa kitu cha msingi sana kulinda kipaji chake ; nidhamu. Huwezi kuondoka eneo la kazi bila kibali sahihi cha kiongozi wako lakini pia kuitikia wito nakuonesha kujali ni jambo lingine ambalo linachangia katika uwajibikaji. Yawezekana kabisa klabu ikawa haijamtendea haki katika matibabu yake kulingana na uhitaji sahihi wa matibabu ya jeraha husika lakini kuonesha nidhamu na kujali kile kidogo ambacho klabu inajituma katika ukata mgumu kama huu ni jambo la kushuku...

HUYU NDO PATO NGONYANI ALEWATOA MCC KIJASHO

Image
PATO NGONYANI AIPA YANGA GOLI 9! Moja ya nafasi ngumu katika soka ni kiungo cha chini. Hii ndio nafasi ambayo inaleta uwiano wa timu katika kujilinda na kushambulia. Roy Keane moja ya viungo bora kuwahi kutokea duniani akitamba sana na kikosi cha Manchester United eneo la kiungo cha chini aliwahi kusema ; " kiungo mkabaji ndio moyo wa timu. Ubora wake uwanjani unawafanya wenzake kutimiza vyema majukumu yao uwanjani " Kwa mtazamo huo, Pato Ngonyani amekuwa na mchezo mzuri kila anapopata nafasi ya kucheza na kutimiza majukumu yake kama ' moyo wa timu'. Pato Ngonyani huu ni moja ya viungo wa Yanga ambaye hana nafasi ya kudumu kwenye kikosi cha kwanza . Ana wastani wa kucheza mechi kati ya 3 mpaka 7 katika mzunguko wa mechi 30 katika ligi kuu. Licha ya uchache huo ameendelea kuaminika katika kikosi cha mabingwa hao watetezi wa ligi kuu nchini kutokana na uwezo wake uwanjani anapopata nafasi. Yanga SC msimu huu wamekuwa na tatizo kubwa la majeruhi na wachezaji ...

MABINGWA LIGI KUU TANZANIA TANGU KUANZISHWA KWA LIGI KUU 1965

Image
MABINGWA LIGI KUU TANZANIA TANGU KUANZISHWA KWA LIGI KUU 1965 Young Africans SC mara 27 Simba SC mara 18 Mtibwa Sugar mara 2 Mseto mara 1 Cosmopolitan mara 1 Coastal Union 1 Tukuyu 1 Pan Africans mara 1 Azam mara 1 Kuanzia mwaka 1965 mpaka 1982 ligi hii ilikuwa ikijumuisha timu za Tanzania bara na visiwani baada ya hapo kila shirikisho kuendelea na ligi yake, FAT ( sasa TFF ) kwa upande wa Tanzania bara na ZFA kwa upande wa Zanzibar. Kwa mtazamo huo Young Africans wanabaki mabingwa wa kihistoria nchini. Ligi hii mwanzoni ilijulikana kama ligi daraja la kwanza ( sasa ligi kuu ) Na samuel samuel

USAJIRI YANGA KATIKA DIRISHA DOGO UZINGATIE HAYA

Image
MTAZAMO WA DIRISHA DOGO LA USAJILI NA TIMU 16 ZA LIGI KUU ....inaendelea MTAZAMO WA Mwanasoka SAMUEL SAMUEL 2. Yanga SC Hawa ni mabingwa watetezi wa ligi kuu Tanzania bara kwa mara tatu mfululizo wakifanya hivyo 2014-15, 2015-16 na 2016-17 lakini pia wakisimama kama mabingwa wa kihistoria wa ligi hiyo kwa mara 27 toka kuanzishwa kwake mwaka 1965 . Kwa misimu kadhaa Yanga SC wamekuwa vyema katika usajili kwa maana ya kuandaa timu nzuri katika mapambano ya ligi hii ndio maana kwa sehemu kubwa wameweza kuitawala ligi kwa muda mrefu ingawa changamoto kubwa ni michuano ya kimataifa . Msimu huu wa 2017-18 ni moja ya msimu ambao mabingwa hawa hawakufanya usajili wa kutisha kama ilivyo ada zaidi ya kurekebisha mikataba ya wachezaji waliopo , kuziba mapengo muhimu yenye ulazima mkubwa mfano eneo la kiungo walipowanasa Pappy Tshishimbi toka Congo, Rafael Daudi wa Mbeya City, Piusi Buswita wa Mbao FC na kiungo huru Buruan Yahya . Sambamba na hilo ni kuimarisha safu ya ulinzi kwa kums...

TIMU ZIFANYE HAYA KATIKA DIRISHA DOGO LA USAJIRI ILI KUJIWEKA SAWA

Image
SAMUEL SAMUEL  MTAZAMO WA TIMU 16 ZA LIGI KUU KATIKA DIRISHA DOGO LA USAJILI Naanza na Simba SC Eneo la ulinzi Dirisha dogo la usajili hawana kazi kubwa sana katika eneo hili ni kiasi cha kutathimini majeruhi ya Shomari Kapombe na mustakabali wao kama timu hususani kwenye mechi za kimataifa kombe la Shirikisho. Ubora wa Erasto kulia sambamba na Ally Shomari bado wanaweza kuliziba vyema pengo lake . Erasto ni moja ya usajili makini ambao Simba walifanya; kimbinu ni mchezaji kiraka kutawala eneo lote la nyuma pia kiungo cha chini. Eneo la kiungo Ni eneo ambalo wapo vyema sana kuliko eneo lolote lakini kuna mabadiliko yanatakiwa kufanyika . Siioni nafasi ya Jamali Mnyate ndani ya klabu hiyo. Huyu wamtoe kwa mkopo kufungua nafasi ya wengine au kubaki na wachezaji wachache ambao kocha anaweza kuwatumia vyema . Ndemla kama atafanikiwa Sweden ni jambo la kheri ili kijana Mohamedi Ibrahim apate nafasi ya kucheza . Muunganiko wa Mkude, Kotei , Muzamiru , Ibrahim, Kichuya na Har...

MACHUNGU YA WANASIMBA TETESI ZA MO KWENDA YANGA

Image
kumbukwe kwa sasa Mohamed Ibrahim almaharufu kama "MO" wanavyopenda kumuita Wanamsimbazi hao amekuwa guzo kubwa mitandaoni na hata kwenye vyombo mbalimbali vya habari akihusishwa kutimkia Yanga Sc ambao wanahitaji huduma ya mchezaji huyo tokea akiwa Mtibwa Sugar ya pale Morogoro inayocheza ligi kuu. Kutokana na Sintofahamu inayoendelea ndani ya Simba na hata kwa mchezji mwenyewe inaonyesha MO akiwa na furaha japo kuna picha mbalimbali zikimuonyesha kama MO amekuwa hana furaha ndani ya Wekundu wa Msimbaza. Kutokana na hali hiyo mmoja wa Wapenzi wa soka ameweza kuonyesha hisia zake kwa MO na hata alipondokewa na Ajibu kwenda Yanga na wachezaji wengine akiwataja  pia ......... Mpenda soka huyo anaeleza kwa machungu jinsi gani anavyomkubali MO na jinsi gani uongozi unavyowatesa mashabiki hao. Hata hivyo inaonyesha habari hizo ni za uongo za MO kwenda Yanga Sc....... Na, BARAKA MBUBA, ........."Nimeona wadau wengi wa SIMBA wakipinga kuondoka kwa "mo"...

MAJIBU YA KAPOMBE KWA ZAKARIA HANS POPE

Image
" Shomari ni muoga tu ... hatuwezi kuvumilia kumlipa bure mshahara ... anatakiwa kucheza sivyo tutamuacha... vipimo vinaonesha mzima ..." Kauli ya mwenyekiti wa usajili Simba SC ndugu Hans Pope juu ya majeraha ya muda mrefu ya beki wa kulia wa timu hiyo Shomari Kapombe. Simba ilimsajili mlinzi huyo toka Azam FC lakini ameshindwa kuichezea timu hiyo kutokana na majeraha ya muda mrefu. Pope amaefanya mahojiano na kituo cha redio cha EFM " kama wanataka kuvunja mkataba wavunje ....mie bado naumwa na daktari kaniambia huenda nitaanza kucheza mzunguko wa pili sasa kama yeye anaongea na vyombo vya habari bila kuniuliza mimi mie sijui hilo . Mie siogopi kucheza... nishacheza sana sasa mtu kusema naogopa kucheza simuelewi" Shomari Kapombe   Beki wa kulia wa Simba SC akijibu tuhuma za Zakaria Hans Pope ! EFM Sports HQ

DALILI ZA BANKA KUTUA YANGA ZA ANZA KUONEKANA

Image
Huku habari zikisema Simba na Yanga zinapigana vikumbo kumuwania Mohammed Issa ‘Banka’, klabu ya mchezaji huyo Mtibwa Sugar imesema ruksa kiungo huyo kuondoka ila afuate masharti. Pamoja na Simba kuhusishwa na mchezaji huyo, kiufundi Yanga ndiyo yenye nafasi kubwa ya kumsajili kiungo huyo kutokana na uhaba wa wachezaji wa aina yake iliyonayo kuliko Simba. Kocha wa Mtibwa Sugar, Zuberi Katwila amesema; timu yoyoye inayomuhitaji kiungo huyo ifuate taratibu za uhamisho ambazo zinafahamika na wao hawana kinyongo. Mtibwa ni klabu ambayo imekuwa ikitoa wachezaji wengi na wenye vipaji kwenda timu kongwe za Simba na Yanga kwa miaka kadhaa sasa. “Banka ni mchezaji wetu halali, hivyo kama kuna timu inamuhitaji taratibu zinafahamika cha msingi wafuate hizo taratibu na siyo kupitia njia ambazo si halali. Hatuwezi kuzuia riziki yake. “Hata mchezaji mwenyewe anajua mkataba wake unasemaje na sisi na kama akipata timu nini anatakiwa kufanya, hatuna tatizo naye na hata timu inayomuhi...

MALALAMIKO MCC KUHUSU GOLI LA KICHUYA YATU BODI YA LIGI NA TFF

Image
Mbeya city wakata rufaa bodi ya ligi maamuzi ya mechi yao na Simba SC jumapili ya tarehe 5 November 2017. Rufaa hiyo inaelezea kutoridhishwa na goli walilofungwa dakika ya 7 na Shiza Kichuya. Wanalilalamikia kwamba ni goli la kuotea ! Note Uongozi wa timu ya Mbeya City umeandika barua Bodi ya Ligi ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kulalamikika kutotendewa haki katika mchezo wao uliopita wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara dhidi ya Simba SC. Mbeya City ilichapwa 1-0 Jumapili na Simba, bao pekee la Shiza Ramadhani Kichuya katika mchezo wa Ligi Kuu Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya. Mtendaji Mkuu wa Mbeya City, Emmanuel Kimbe amesema kwamba uchezeshaji wa refa Ahmed Kikumbo aliyesaidiwa na Omar Juma wote wa Dodoma na Michael Mkongwa kutoka Njombe haukuwa wa haki kwa mujibu wa sheria 17 za soka. Bin Zubery

MKUMBUSHENI MANARA MPIRA SIO MCHEZO WA MALAIKA

Image
Mkumbusheni Manara, mpira sio mchezo wa Malaika Kalamu ya Ally Kamwe ANAWEZA kuwa sawa kwa staili yake ya ufanyaji kazi. Kama viongozi wa Simba ambao ndio mabosi wake wanaridhishwa naye, mimi ni nani hadi niuponde utendaji wa Haji Manara? Sina tatizo na kazi ya Manara pindi anaposimama na kuizungumza Simba. Tatizo langu linakuja pindi anapojaribu kuufanya mpira wa miguu uwe mchezo wa malaika. Si sawa hili. Kama tukishindwa kumwambia sasa, tutapata shida sana kumweleza baadaye wakati akiwa ameshapata kundi la wafuasi wa kumwamini. Haji anakosea sana kuchanganya mapungufu ya marefa kwenye maamuzi yao na hila za kuiumiza klabu yake. Hivi ni vitu viwili tofauti. Nitakwambia kwanini. Tangu aingie madarakani, Rais wa Fifa, Gianni Infantino, amekuwa akifanya kazi kubwa ya kuingiza matumizi ya teknolojia kwenye soka kwa ajili ya kusaidia waamuzi. Lakini mwisho wa siku changamoto zimekuwa nyingi kuliko faida. Kwanini? Sababu ni rahisi sana, soka ni mchezo wa binadamu. Udhaifu w...

GOLI LA SIMBA DHIDI MCC NA MAONI YA WADAU NCHINI; UJUMBE KWA MANARA

Image
Nategemea tena kumskia msemaji wa offside fc akiongelea ubovu wa waamuzi wa tz baada ya mbumbumbu fc kufunga goal la kuibia. Nategemea albino atahitisha kikao na waandishi wa habar kuongelea goli walilopewa mikia fc dhidi ya mbeya city hii leo kwenye uwanja wa sokoine jijini mbeya. Sijui waamuz hawa wanatupeleka wap na huu ujinga wao. Kocha wa mbeya city hajaamini kama hawa waamuzi wamekaa darasani kusomea hiyo koz yao maana ni madudu zaid ya madudu kwa soka la tz. Hongereni offside fc kwa kubebwa leo. Haya Sasa We Bwege Leo Chukua Tena Smart Phone Na Tv Uaite Waandishi Wa Habar Uwaoneshe Lile Goli Alilofunga Ashura Kichura Chura Na Umwandikie Barua Waziri Wa Michezo Kwamba Leo Refa Kawabebeni Kwa Kuwapa Goli La Off Abdala Maana Kwenye Offside Ilipitiliza Kabisa ''HAWA VUVUZELA FC BAADA YA KUSHINDA MECHI YA LEO WANAFURAHI NA KUDAI KUWA WANAUWEZO WA KURUKA MAGHOROFA BAADA YA KUTOROKA PORINI, MNAJIDANGANYA WENYEWE TUPO ENDELEENI KUKAIMU CHEO CHETU. MNAJUA ITAKUWAJE SUBIR...

NI LWANDAMINA VS HANS VAN PLUIJM LEO

Image
LWANDAMINA VS HANS VAN PLUIJM JUMAMOSI HII Jumamosi hii wapenzi wa ligi kuu Tanzania bara wanakwenda kushuhudia moja ya mechi yenye gumzo la aina yake ambayo toka kuanza kwa ligi ilikuwa ikisubiriwa kwa hamu kubwa . Hii ni mechi kati ya mabingwa watetezi Yanga dhidi ya wageni wa ligi Singida United itakayopigwa katika dimba la Namfua mjini Singida baada ya kufanyiwa ukarabati mkubwa wa kupandwa nyasi upya sehemu ya kuchezea . Hans Van Pluijm kocha mkuu wa Singida United kwa mara ya kwanza anakutana katika ligi kuu na timu ambayo kwa nyakati tofauti ameifundisha na kuipa mafanikio makubwa . Hans Van Pluijm mwenye falsafa ya soka la kidachi kushambulia muda wote , aliweza kuipa Yanga vikombe viwili vya ligi kuu Tanzania bara , Ngao ya jamii , Azam Sports Federation Cup na msimu wa 2016 kuwafikisha hatua ya makundi kombe la Shirikisho barani Afrika . Huyu ndie aliyemwachia kijiti George Lwandamina ambaye anaionoa Yanga SC kwa sasa akiwa tayari ameendeleza wimbi la ushindi kwa kuw...

SHAFII DAUDA vs HAJI MANARA PART II

Image
October 31, 2017 afisa habari wa klabu ya Simba Haji Manara alifanya mkutano na waandi wa habari za michezo, katika mkutano huo Manara alitumia muda mwingi kulalamikia baadhi ya maamuzi yaliyofanywa na waamuzi katika mechi kadhaa (Mbao vs Simba, Stand United vs Simba, Yanga vs Simba) akidai waamuzi wamekuwa wakiikandamiza klabu yake. Manara alikwenda mbali na kuwashutumu wanahabari (wachambuzi) kwamba hawaandiki wala hawasemi pale klabu yake inapokuwa imeonewa badala yake wanasifia upande wa pili. Kwanza kabisa mimi sijui nafasi ya Haji Manara kwenye klabu ya Simba, kwa sababu mara nyingi amekuwa akizungumzia masuala ya Yanga pamoja na vilabu vingine tofauti na maafisa habari wengine wanavyofanya pindi wakikutana na waandishi wa habari. Kwenye mkutano wake nilisikia akimzungumzia afisa habari wa Yanga Dismas Ten. Manara alikuwa akijinadi yeye ni afisa habari wa klabu kubwa hadi mashabiki wa Yanga walimkimbilia baada ya kumalizika kwa mechi ya watani wa jadi. “Juzi tumemaliza m...